Saturday, August 23, 2014

MAZUNGUMZO YA MARK SCHROEDER NA RAIS KIKWETE




Mark Schroeder: Hello, I'm Mark Schroeder, Vice President of Africa Analysis at Stratfor. I had a recent conversation with the President of Tanzania, Jakaya Kikwete, following his participation at the recent U.S.-Africa Summit that took place in Washington, D.C. President Kikwete describes his vision for Tanzania for the years to come.
---
Mark: You joined us in Texas immediately following the historic United States-Africa Summit, the first time that the United States government has hosted such a summit. Could you describe your observations of the U.S.-Africa Summit that just concluded in Washington?
President Jakaya Kikwete: What I can really say is first, my deepest appreciation to President Barack Obama for conceiving the idea of hosting this summit. We have been exposed or we have had an opportunity to meet the mega players in the U.S. economy. These are companies that have not been easy for African heads of state and government to get access to. And this is really a game-changer, because what is it that we are looking for from Africa? Well it's for promoting investments, promoting trade, we're looking for technology, we are looking for skills, transfers, and this summit has made it possible to create the ambience for the realization of this dream.
Mark: From a political standpoint, the country is a significant role model in the region, in the East African region on the continent and abroad, but the country really models stability. We have seen, unfortunately, conflict in other countries of the region, but could you tell us what are the characteristics of Tanzania that has really modeled stability in that country and really sets that country apart?
President Kikwete: I think it's the pursuit of sound political and economic policies in the sense that politics and economic policies that have been inclusive. Nobody is being discriminated against or being denied the right to access the political or economic because of his ethnicity or because of his tribe, because of his religion or the part of the country that he comes from or because of his gender. I think our first leader really created the foundations for this. He made it clear that if we discriminate each other on the basis of ethnicity, religion, color of the skin or tribe or the area that we come from, we are going to tear apart the country. So, he laid these foundations and fortunately the successive leaders have maintained this policy, have advanced this policy, and it is actually in my view what has really delivered.
Mark: If I could just ask you Mr. President, if you could describe the infrastructure program that you have, once again, that really enables Tanzania to position itself in two regions, the East Africa region, the Southern African region, but as a part of this greater Indian Ocean base as well connected to South Asia, East Asia, it's a really dynamic, large region. Could you describe Tanzania's position there?
President Kikwete: Especially ports, which is a very critical factor for us. The port of Dar es Salaam, we are building two new berths, Berth 13 and 14. We are operating the seven berths, Berth number one through seven, which because we a re looking for support from our development partners but we are also leveraging private sector participation on a PPP basis to develop these ports. Then of course these ports, Tanzania is situated in, the geography of Tanzania is another resource of this kind. We are bordering Uganda, Rwanda, Burundi and the Democratic Republic of the Congo, Zambia, Malawi that have been using the port of Dar es Salaam.
Mark: Yes.
President Kikwete: So we now have to deal with the railways, where the central corridor which links the port of Dar es Salaam with Uganda, Rwanda, Burundi, and the Democratic Republic of the Congo, we're upgrading that one from a narrow gage to a standard gage. Then we are extending the railway line into Rwanda, onward to the Congo, into Burundi and onward again to the Congo. The standards have been completed. It will cost us about $4.1 or 4.2 billion. So there is so much on the infrastructure side that the way we are doing, but why are we doing it? Because we are seeing poor infrastructure impedes growth and development in a big way. We are building 11,000 kilometers of optic fiber, and nationwide optic fiber network. The whole of the eastern side of the African continent is not being connected to the international information highway. There is no optic fiber network submarine linking that. Now South Global has built what we call the SEACOM. It has landed south of Dar es Salaam, but as we are planning to do that we also started working on the nationwide optic fiber network so that when a submarine cable lands in Dar es Salaam we will be able now to make use of it and connect the country to this cable so that we get into the super highway.
Mark: In one advisory study that Stratfor has done, called the Post-China 16, it has really identified Tanzania because of those qualities, because of infrastructure developments, Tanzania has been set apart. The last word to you, Mr. President, is you have intimated the bright future for Tanzania. If you could just conclude with the word of Tanzania in a few years to come, please tell us.
President Kikwete: The other objective is to develop Tanzania into a middle-income country by 2025. By the year 2025, we will have the GDP per capita of $3,000. That's one, but also a highly educated and highly skilled population, we call a knowledge society, a highly knowledge society. Increase the productivity of the country. Make it a country semi-industrialized economy, but competitive enough. Then of course, we are also the fourth to put on, in fact to here, has been also ensure the country is well-governed, good governance, rule of law, human rights and all these vices in society are being fought mercilessly. So these are the four main objectives. It's a tall order, it looks not feasible, but when we started with about $300 GDP per capita, we are now close to $800. So I believe in the remaining ten years we will be able to get there and now of course there is natural gas coming in, coming on stream. It should certainly open up now the opportunities for the growth of the economy. So I'm really saying the future is going to get to a middle-income country by 2025. It's a tall order but I think with the long-term perspective plan we have the road map, we have the benchmarks. I'm optimistic that we can gradually become a middle-income country.
Mark: Thank you President Kikwete that has been a tremendous conversation, and really under your leadership Tanzania has achieved so much already but with the plans that you have initiated that you have just described to us with the resources that are being mobilized from a human capital basis, from an economic development basis, the future for Tanzania is bright. It has been an honor to host you here in Texas at the Stratfor offices. It has been an honor to have you after the historic U.S.-Africa Summit. Thank you again for being on the Stratfor conversations program President Kikwete.
President Kikwete: The pleasure is mine. Thank you. Thank you for having me here. Thank you for the support. We look forward to continued cooperation with Stratfor.
Mark: Thank you sir.




HONGERA BEN SAANANE

Maamuzi Rasmi juu ya barua yangu ya mgogoro wa kikanuni/masharti ya uchaguzi wa baraza la vijana Chadema(BAVICHA) Taifa yamefanyika.
Fomu za uchaguzi zilizotolewa tarehe 12/08/2014 , liliwekwa sharti kuwa mgombea awe na miaka 18-30(Awe amezaliwa 1984 na kuendelea).
Sharti hili lililowekwa kwenye mabano lilinisukuma ku-challenge kanuni/masharti/mahesabu hayo pamoja na masharti mengine kwa kufuata taratibu za chama kama nilivyowaeleza na nikaahidi kusubiri uamuzi
Hoja yangu ilikua kama aliyezaliwa tarehe 01.01.1984 ana haki ya kugombea kwanini isiwe mimi niliyezaliwa tarehe 13/12/1983 yaani wiki mbili na nusu kabla yake kwa kuwa hadi siku ya uchaguzi atakua na miaka 30 na miezi 9 na siku 10 wakati mimi nitakua na miaka 30 na miezi 9 na siku 28 halikadhalika yule aliyezaliwa tarehe 11/09/1983 atakua na miaka 30 na miezi 11 na siku 30 hadi siku ya uchaguzi tarehe 10.09.2014.
Na kwamba ingekua sahihi kama sharti hilo "SHARTI NDANI YA MABANO" lingetamka sawi kuwa mgombea asiwe amefikisha miaka zaidi hadi ifikapo siku ya uchaguzi.Hii ndio ilikua hoja yangu.
Nilirejea katiba na miongozo yetu na kanuni za uchaguzi uliopita wa Baraza la Vijana uliofanyika Mwezi Mei 2011.
Maamuzi ni kuwa wagombea waliozaliwa kuanzia mwaka 1984 ndio watakaokuwa eligible kugombea kama inavyoonekana kwenye fomu zitakazojazwa na wagombea na zipo pia kwenye tovuti ya chama.
Kutokana na maamuzi haya nasikitika kuwatangazia vijana wenzangu kuwa ,kufuatia "SHARTI HILO NDANI YA MABANO " NIMEJIENGUA RASMI KATIKA KINYANG'ANYIRO CHA UCHAGUZI KUWANIA NAFASI YA JUU KUONGOZA BARAZA LA VIJANA CHADEMA (BAVICHA).
Maandalizi mliyonishauri niendelee nayo wakati nasubiri uamuzi yatasitishwa
Maandalizi yote ya mkutano na waandishi wa habari kesho Travertine Hotel tumeyasitisha rasmi,Maandalizi ya kurejesha fomu jumatatu ambayo jeshi la polisi liliarifiwa na kukiri kupokea barua iliyoandikwa na vijana waliotaka kunisindikiza kurejesha fomu kuanzia viwanja vya BIAFRA kuelekea Makao makuu yamesitishwa.
Kwa moyo wa kipekee na kwa unyenyekevu mkubwa,nawashukuru marafiki zangu wa karibu na wa mbali,nawashukuru marafiki wa BAVICHA kwa maandalizi kabambe ya kampeni,Nawashukuru ninyi marafiki zangu hapa Facebook na mitandao mingine kwa kuniunga mkono kwa wingi wenu na kujitolea kupambana na dhuluma na hila chafu chafu za watu wachache sana waliokua wakifanya siasa chafu katika safari hii.Mlijitolea kulinda haki,misingi na falsafa ya chama chetu na pia principle zenu kwa kile mnachoamini bila woga.Mlisimama kidete
Ninyi mmekua Nanga yangu initulizayo katika dhoruba.
Ninatambua thamani na mchango wenu kwangu.
Kuna wale walioomba kuchangia kampeni na ziara yangu,ziara ya kufufua ndoto ya mashujaa wetu na kuitaka/kuirudisha Tanzania (Reclaiming Tanzania ).
Sina cha kuwalipa. Nawashukuru sana kwa kusimama nami . Mwenyezi Mungu awajalie kila lililo la kheri nanyi.
Ninafarijika na kuona fahari kuwa chama chetu kimekua sambamba na kasi ya ukuaji wa Teknolojia pengine kuliko chama kingine nchini.
Haikushangaza sana kuona idadi kubwa ya viongozi waliochaguliwa kwenye majimbo na wilaya na hasa tuko nao hapa na kwenye mitandao mingine kama Watsap.
Hakika kampeni za uchaguzi huu tungefanya mageuzi makubwa ya matumizi ya mitandao katika siasa.
Wale wote waliong'ang'ania fikra za ukale(Primitive mentality) tungewaziba midomo.
Mara kadhaa kupitia mitandao hii na ana kwa ana nimekua nikihimiza wale wote wenye nia na dhamira ya kupigania mabadiliko wajitokeze kwa wingi kugombea nafasi za uongozi.
Wengi walifanya hivyo na walishinda kwa kishindo na hata chaguzi za mikoa.
Chama chetu kimekua kuliko wakati mwingine wowote.
Chama ni kikubwa kuliko sisi.Tukilinde kama mboni ya jicho .
Kukilinda CHADEMA hata kujitoa sadaka binafsi,ni Sadaka kwa Mageuzi na sadaka hii ni hazina isiyooza kwa vizazi vijavyo vya watanzania.
Mwenyezi Mungu atulinde.
Tusikubali kuingia katika majaribu au mitego yoyote itakayotugawa.Tusikubali kuwa katika upande mbaya wa historia ya harakati za mageuzi.
Safari bado ni mbichi,tutizame tulikotoka na kisha tutazame mbele.Wapo waliofukuzwa /kunyimwa kazi (Mimi ni mmojawapo) ,walioachwa ,waliojeruhiwa na kupata ulemavu na waliopoteza maisha kwa ajili ya CHADEMA na kutafuta haki za kiraia.
Tuendelee kujiimarisha kama taasisi na ni rai yangu kuwa ukomavu wa kisiasa unahitajika zaidi kutokana na ukweli kuwa uchaguzi ndani ya chama ni mgumu kuliko unapopambana na wagombea kutoka nje ya chama.
Ni katika uchaguzi kama huu ,marafiki na mahasimu watajipambanua lakini kitu bora na cha muhimu zaidi mahasimu wanapoonyesha uhasimu katika hoja huwaimarisha wote pamoja na taasisi tofauti na wale wenye siasa za mitaroni.Hao ni kuwapuuza na kusonga mbele.
Tuendelee kuogelea kuelekea kina kirefu zaidi.
Wale wenye hila na nia ovu kama mlivyoshuhudia siku za karibuni,wasisahau kuwa tutaendelea kukutana kwenye kordo za siasa.I'm there to stay.
Sitawafuata kwenye huko vichochoroni kwenye mitaro ya "SIASA MAJITAKA".
Historia kwangu sio gereza,bali ni darasa.Kuna wale waliowahi(labda Walitabiri) na kuandika kwenye mitandao ya kijamii hata kabla fomu hazijatolewa kuwa Mwisho wa Ben Saanane Umefika.Wajitafakari Upya.
Uamuzi huu Sio alama ya Nukta,Bali ni alama ya Mkato Katika Safari yangu ya Kisiasa.Wala sio alama ya Mabano.
Nilipoenguliwa uchaguzi wa BAVICHA mwaka 2011 kwa tuhuma za kuunda Alliance haikua alama ya Nukta katika Safari Yangu.
Nilipoadhibiwa na Baraza la Vijana ambapo mojawapo ya makosa ilikua kutoa tuhuma za usaliti hadharani dhidi ya aliyekuwa naibu katibu Mkuu Zitto Kabwe Tarehe 5 January 2013 na kuzuiwa kugombea nafasi yoyote ndani ya baraza la vijana kwa muda wa mwaka 1 haikua alama ya nukta, bali ilikua alama ya mkato katika safari yangu kisiasa.
Kama nilivyowaahidi ,nitaendelea kukilinda na kukijenga chama chetu na safari hii ya mapambano imezidi kutiwa chachu.
Kuna kisa kimoja cha kifalsafa kwenye Biblia.Kisa cha Mama aliyeiba Mtoto na kesi kupelekwa kwa mfalme Sulemani baada ya utata mkubwa juu ya mams halisi wa mtoto na baina ya wanawake wawili waliokua wanamgombania.Aliamuru Panga liletwe mbele yake kisha mtoto akatwe ili wagawane sawa.Mwanamke Mmojawapo akaridhia haraka wakati mwingine alijibu 'Ewe Mfalme,Ni bora akabidhiwe huyu mwenzangu ' Busara zikamtuma Sulemani kuwa Mama halisi ni yule mwenye uchungu na mtoto.Tusiruhusu sasa kuingia upande mbovu.
Nimepokea Ushauri mwingi kutoka kwa ndugu,jamaa na marafiki .Msiumie kwa uamuzi huu,tuuheshimu .
Tutaendelea kuwaabisha wale wote wa nje wanaotazama uchaguzi wetu wa ndani kwa jicho la husuda.Maadui wa demokrasia na haki tutawashinda kwa ukomavu wetu wa kisiasa tu.
Kaka yangu Godbless Lema na baadhi ya wabunge vijana na madiwani wetu, nimeheshimu Ushauri wenu.Dada yangu Halima Mdee nimeendelea na nitaendelea kuheshimu ushauri wako.
Nina maamuzi mengine nitakayochukua baada ya kutafakari kwa kina ndani ya saa 48 zijazo.
Mwanamapinduzi Ninayemuhusudu sana Rais wa Zamani wa Venezuela Hugo Chavez alishawishi na ameendelea kunichochea kwa kauli yake kwenye nukuu siku siku zote "There is no turning Back".
Mwenyezi Mungu awabariki nyote.
Aluta Continua ,Victory Ascerta....


CHANZO MTANDAO WA WANABIDII.

Wednesday, August 6, 2014

SALAMU ZA ACT- Tanzania

SOTE NI WATANZANIA

Ndugu Viongozi wa vyama vya siasa nchini, wanachama wa vyama mbali mbali vya siasa nchini, wadau mbali mbali wa siasa nchini na watanzania wote kwa ujumla; tunapenda kuwasalimu kwa salamu inayoashiria mabadiliko na uwazi!

Chama cha ACT-Tanzania kinapenda kuwapa salamu hizi kufuatia wasi wasi ambao umekuwa ukioneshwa na baadi ya Viongozi wa vyama vya siasa, wanachama wao na hata washabiki wao juu ya ujio wa Chama kipya cha ACT-Tanzania.Kumekuwa na wimbi la baadhi ya watu kutoka vyama kadhaa vya kiaisa kulalamika kwamba eti chama cha ACT-Tanzania kimekuja kuwamaliza kisiasa.

Chama cha ACT-Tanzania kinapenda kutuma salamu kwa vyama vyote vya siasa nchini na wanachama wao kwamba; Chama cha ACT-Tanzania hakijaja Kuvimaliza vyama vyao wala kupambana na mtu yeyote wala chama chochote cha siasa nchini, bali kimekuja kupambana na matatizo sugu yanayomkabili mtanzania kupitia misingi, falsafa na itikadi zake.ACT-Tanzania imeanzishwa katika misingi yake yenyewe, Inajijenga katika misingi yake yenyewe,Itajiimarisha katika misingi yake yenyewe, Itatembea katika misingi yake yenyewe, Itasimama katika misingi yake yenyewe na kama ni kuanguka; basi itaanguka kwa kutokusimamia misingi yake yenyewe.Uwepo wa ACT-Tanzania hautegemei wala hautatagemea uwepo wa vyama vingine au operesheni za vyama vingine.Kwa lugha nyingine ni kwamba uwepo wa ACT-Tanzania hautategemea matukio bali misingi yake yenyewe.

Hata hivyo, kwa kuwa lengo kuu la ACT-Tanzania ni kupambana na matatizo sugu yanayomkabili mtanzania ambayo bado yanasumbua sana na kuleta machungu katika maisha ya watu, ili kuleta unafuu na furaha katika maisha ya mtanzania; lengo hili litafikiwa kwa ukamilifu wake kwa chama kupewa mamlaka ya kuiongoza nchi.Mamlaka hayo yatatoka kwa wananchi watakaoikubali misingi itikadi na falsafa za chama.Kwa kuwa katika uchaguzi chama kinachoshinda ni kimoja, ni wazi kwamba ACT-Tanzania itakaposhinda; vyama vingine vyote vitabaki kuwa vyama vya upinzani wakati ACT-Tanzania ikisimamia itikadi yake na ikitekeleza sera zake lakini hii haimaanishi kwamba ACT-Tanzania imekuja kuvipoteza vyama hivyo katika sura ya siasa za Tanzania! kwani hilo sio lengo la msingi la ACT-Tanzania.

Kadhalika tunafahamu kwamba kutokana na ubora wa falsafa, misingi na itikadi za ACT-Tanzania, Uwajibikaji,uwazi na uadilifu wa viongozi wa chama tulionao na tutakaokuwa nao, wanachama wengi kutoka vyama vyote nchini, watakuwa wakijiunga na ACT-Tanzania makundi kwa makundi.Hata hivyo hiyo haitakuwa inamaanisha kwamba tuna uadui na vyama wanakotoka wanachama hao.Tutafanya nini sasa! katika hali hiyo ndipo tunaposisitiza kwamba itatupasa tuwe na uvumilivu wa kisiasa.Tunawashauri wale watakaoona kwamba chama chetu kinafanya vizuri, wasitujengee uadui bali watuunge mkono au watuvumilie tu.

Kuhusu watu wanaotumia mitandao ya kijamii na vyombo vingine vya habari kudai kwamba wao ni wana ACT-Tanzania, na chama hiki kimekuja kupambana na watu fulani fulani, nao wanasema kwa niaba ya chama! na watu wanaotunga habari na kudai zimesemwa na viongozi wakuu wa chama kwamba ACT-Tanzania imekuja kwa lengo kuu la kuua vyama vya watu fulani,Tunawaomba watanzania muwasamehe kwani kuna siku watajua kwamba wanachokifanya si sahihi na wakarudi kwenye njia ya ukweli na ustaarabu.

Mwisho, ACT-Tanzania kupitia Ofisi yake ya Mawasiliano na Uenezi, Inajenga na itaendelea kuimarisha mahusiano na vyama vyote nchini kwa kadiri itakavyowezekana kwani chama kinaamini kwamba sote ni watanzania na zaidi ya hapo sote ni watu.Chama kinakaribisha na kinapokea ushauri wowote kutoka kwa yeyote bila kujali chama chake, kitaupitia na kuuchambua na kila itakapoonekana unafaa, utafanyiwa kazi.Chama kiko tayari kushirikiana na yeyote anayependa ushirikiano katika mambo mema na yenye tija kwa taifa.ACT- Tanzania bado ndio chama kidogo zaidi nchini, hivyo badala ya kukiogopa; ni bora kukishika mkono ili kuimarisha demokrasia.Kadhaalilika Chama kupitia Ofisi ya Mawasiliano na uenezi, kitajenga na kuimarisha uhusiano na vyama mbali mbali duniani hasa vile vyenye muelekeo wa "Mrengo wa Kati Kushoto".

Ikumbukwe kuwa ACT-Tanzania ni kwa ajili ya taifa la leo na kesho.

ACT- Tanzania ..............Taifa kwanza!,

Mabadiliko na uwazi...........Chukjua hatua!


Imetolewa na Ofisi ya Mawasiliano na Uenezi ya Dar es Salaam leo tarehe 05/06/2014.

Friday, September 27, 2013

MPANGO WA USHAURI WA BIASHARA

CPM Business Consultants imeandaa mpango kabambe wa ushauri wa biashara (Mentorship) kwa wafanyabiashara wadogo wa kati na wakubwa na wale wanaotaka kuanzisha biashara ili kuwawezesha kuwa wafanyabiashara wakubwa na wenye mafanikio. Mtu atakakayejiunga na mpango huu atapewa mbinu za hali ya juu za biashara na uwekezaji ambazo zitamuwezesha kuinuka kiuchumi na kuwa mfanyabiashara mkubwa kwa haraka. Mtu yeyote anaweza kujiunga na mpango huu ambao mkataba wake utakuwa ni wa mwaka mmoja mmoja ambao unaweza kurudiwa tena.Kwa nini uchague CPM Business consultants? Tumeweza kuwainua wajasiriamali wengi kwa ushauri wetu. Kitabu chetu cha Mbinu za biashara na maarifa ya kupata pesa na utajiri, kimewainua wajasiriamali wengi wengine ndani ya muda wa miezi 6 hadi mwaka mmoja. Pia tumefanikiwa kuuza nakala 4,000 za kitabu hicho kwa kipindi kifupi kwa sababu kinapendwa sana. Tumeweza kuandaa mpango wa biashara/michanganuo kwa wale walioomba mikopo Benki. Katika kipindi cha miaka 3 iliyopita tumewawezesha wateja wetu kupata mikopo ya sh. milioni 400 toka benki.
Manufaa ya kujiunga na mpango huu;
Utapewa mbinu za hali ya juu za biashara na uwekezaji ambazo zitakuwezesha kuinuka kiuchumi na kuwa mfanyabiashara mkubwa kwa haraka.
Utapata kitabu cha ujasiriamali kilichotungwa na Mshauri wa biashara.
Utajiunga na mafunzo maalum ya ujasiriamali kwa email kipindi chote utakachokuwa umelipia michango.
Utapata ushauri kwa kipindi cha mwaka mmoja bila kulipia gharama yoyote na unaweza kumpigia simu mshauri wakati wowote na kupatiwa ushauri.
Utapewa huduma ya kutangaza biashara yako kwenye mtandao wa Internet wenye wateja 50,000 bila gharama ya ziada.
Utapata ushauri wa kisaikolojia na matatizo ya mahusiano na maisha yanayokukabili.
Gharama ya mpango huu ni Sh. 25,000.00 Elfu ishirini na tano kwa mwaka. Ili kuomba kujiunga na mpango huu tuma sh. 25,000 kwa M PESA kwenye simu namba 0755394701, Kwa maelezo zaidi unaweza kupiga simu au kutuma email kwa cnazi2002@yahoo.com
Tumeamua kutoa bei ndogo tofauti na tangazo letu la mwanzo kutokana na maombi ya wadau wengi kuutaka mpango huu kwa gharama ambazo wanaweza kuzimudu.
CHARLES NAZI
MSHAURI WA BIASHARA
CPM BUSINESS CONSULTANTS

Thursday, September 19, 2013

RAIS KIKWETE:ACHENI KUISEMA NA KUIKEJELI TANZANIA

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete amewataka Watanzania kuisemea, kuijenga na kuitetea nchi yao badala ya kushiriki katika kuikejeli na kuidharaulisha.

Rais Kikwete amesema kuwa kuisemea na kuitetea Tanzania ni wajibu wa kila Mtanzania awe anaishi ndani ya nchi ana ughaibuni.

Rais Kikwete amesema kuwa ni jambo la ajabu kuwa kazi ya kuisemea, kuitetea na kujenga jina zuri la Tanzania inafanywa zaidi na watu wa nje kuliko baadhi ya Watanzania na hasa wale wanaoishi nje ya nchi.

Rais Kikwete ameyasema hayo usiku wa jana, Jumatatu, Septemba 16, 2013, wakati alipokutana na kuzungumza na
Watanzania waishio katika Jimbo la California kwenye siku ya kwanza ya ziara yake ya siku mbili katikia jimbo hilo na baadaye  katika sehemu nyingine za Marekani.

Rais Kikwete amewaambia Jumuia ya Watanzania katika Hoteli ya Embassy, San Rafael, California: “Ni wajibu wa Watanzania popote walipo kuisemea vizuri na kutetea maslahi ya nchi yao. Ni jambo lisilo na tija kushiriki katika kuilaumu na kuikejeli nchi yetu. Utasikia na kusoma kwenye mablog baadhi ya watu wakisema kuwa ‘hii nchi gani?” amesema Rais Kikwete.

Rais ameongeza: “Siyo tu kwamba ni wajibu wa kila mmoja wetu kuisemea Tanzania lakini ni wajibu wetu kusaidia kusukuma maendeleo ya Tanzania. Hakuna mtu mwingine wa kuifanya kazi hii isipokuwa Watanzania. Hii ndiyo nchi yetu. Hakuna nchi nyingine hata kama tunailaumu kiasi gani.”

Amesisitiza: “Kama watu wa nje wako tayari kuisemea nchi yetu, nyie mnashindwaji vipi kuifanya kazi hiyo ya kuitetea nchi nzuri hii? Hivi nani tunamwachia aijenge nchi hii, aitetea nchi hii? Wengine wanathubutu kuuliza ‘Nchi nzuri? Turudi’. Hivi nani ulimwachia akujengee nchi nzuri ili uweze kurudi?”

Rais Kikwete amesema kuwa ni lazima Watanzania wajifunze kutoka kwa wenzao, wakiwemo majirani zao kuhusu namna ya kutetea maslahi ya nchi yao kwa kila jitihada.

Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,
Ikulu,
DAR ES SALAAM.

17 Septemba, 2013

Sunday, September 15, 2013

UWEKEZAJI KATIKA GESI NA MAFUTA,MAONI YA REGINALD MENGI

Septemba 7, 2013 nilipokea barua pepe (email) yenye kichwa cha habari kisemacho “ubinafsi/ufisadi wa MENGI na Chuki/Fitina kwenye Maendeleo”.

Aliyetuma email hiyo alijitambulisha kama “CCM TANZANIA” na email ilisambazwa kwa vyombo vya habari, waandishi na watu wengine wengi wakiwamo wanasiasa. Kabla ya hapo nilifowadiwa nakala ya ujumbe (SMS) na watu ambao walitumiwa na Profesa Sospeter Muhongo, Waziri wa Nishati na Madini na Mbunge inayosema;

“Ambieni Watanzania: Kampuni za Mengi zimeshikilia vitalu 59 vya madini vyenye ukubwa wa mita za mraba 3,752.37 (sq km) Amevishikilia, ameshindwa kuviendeleza. Watanzania wanakosa mapato na ajira! Sasa anataka vitalu vya gesi na mafuta. Je huu ndio uzawa?|

Na

“Mengi hana uzawa bali ubinafsi. Anataka kufanya udalali wa vitalu vya raslimali zetu. Waelezeni Watanzania ukweli huu.”

Vile vile Septemba 5, 2013 Profesa Muhongo akijibu swali la Mwandishi wa habari lililouliza;

“Mhe. Waziri tunataka ufafanuzi kuhusu kauli yako ya hivi karibuni kwamba waTanzania hawana uwezo wa kuwekeza katika uwekezaji wa gesi asilia. Kwanza kauli hii ni kweli? Pili kauli kwamba Watanzania wanaweza kuwekeza kwenye sekta ya machungwa tu huoni kwamba si kwamba unawavunja moyo bali unadhalilisha wewekezaji wazalendo?”

Na Profesa Muhongo akajibu:

“Kila mtu alitoa mawazo ya sera ya gesi wakiwemo TPSF. Mengi na wenzake wanataka vitalu wafanye ulanguzi wa gesi na mafuta yetu. Tutatoa orodha ya vitalu vya madini vilivyoko mikononi wa Mengi ambavyo anafanya ulanguzi. Ukweli utaonyesha ubabaishaji na ulanguzi wa Mengi wa genge lake.”


Nimeona ni vyema nitumie haki yangu ya kujibu (right of reply), lakini kwa wale wanaohusika kusambaza taarifa hizo kuchafua jina langu wajue kwamba kujibu kwangu hakuondoi haki yangu ya kuchukua hatua za kisheria.


Kuingizwa kwa vitalu vya madini katika hoja ya gesi

Huo ni upotoshwaji wenye lengo la kututoa kwenye hoja ya msingi ya rasilimali yetu ya gesi. Sijawahi kufanya udalali kwenye vitalu vya madini. Huu ni uongo wa hali ya juu.

Tamko la TPSF na majibu ya Profesa Muhongo

Siku ya Agosti 28, 2013 Tanzania Private Sector Foundation (TPSF) ilifanya kikao chake cha Bodi na baadaye kufanya mkutano na waandishi wa habari. Mambo mengi yalizungumzwa katika kikao hicho ikiwa ni pamoja na uwezeshaji wa Watanzania (Economic Empowerment).

Kuhusu uwezeshaji Watanzania, mambo muhimu matatu yalijadiliwa na kutolewa mapendekezo. Mambo hayo ni 1) Manunuzi ya Umma (Public Procurement); 2) Ardhi na uvuvi; na 3) suala la gesi asilia.

Kwenye mkutano na waandishi wa habari, mimi nikiwa Mwenyekiti wa TPSF, niliwasilisha maoni ya TPSF kuhusiana na Manunuzi ya Umma, wakati Makamu Mwenyekiti wangu, Salum Shamte, aliwasilisha maoni yetu kuhusiana na sekta ya ardhi na uvuvi na mwishoni Mkurugenzi Mtendaji wa TPSF, Godfrey Simbeye, aliwasilisha maoni TPSF kuhusiana na gesi asilia.

Katika maoni yake TPSF ilisisitiza umuhimu wa ushirikishwaji wa Watanzania katika uchumi wa gesi na kushauri kusitishwa ugawaji wa vitalu vya gesi hadi hapo sera ya gesi itakapokua tayari. Mwisho Bwana Simbeye alisema kwamba TPSF itaomba kukutana na Profesa Muhongo kuwasilisha mawazo na mapendekezo ya taasisi hiyo.

Siku chache baada ya TPSF kutoa maoni yake mambo mawili yalitokea. Kwanza Profesa Muhongo alijibu kupitia vyombo vya habari kwamba mpango wa kugawa vitalu vya gesi na kuingia mikataba utaendelea.

Profesa Muhongo pia alisema wazi kwamba hana mpango wa kukutana TPSF, kwani kufanya hivyo ni kupoteza muda. Matokeo yake Profesa Muhongo hajajibu hoja kuhusiana na barua aliyoandikiwa na TPSF. Binafsi nilishitushwa na msimamo wa Profesa Muhongo kwani Serikali ya awamu ya nne imepiga hatua kubwa katika kudhihirisha kuwa ni “serikali sikivu”. Ingemgharimu nini Profesa Muhongo kukaa na kutusikiliza? Hakuna ambacho angepoteza zaidi ya dakika chache za muda wake.

Jambo la pili ambalo lilitokea ni mimi binafsi kushambuliwa kana kwamba maoni yaliyotolewa kuhusiana na gesi ni maoni yangu binafsi na si ya TPSF. 

Mifano ya mashambulizi dhidi yangu ni kama nilivyoonyesha hapo juu katika email na ujumbe mfupi wa simu (SMS).

Msimamo wa Profesa Muhongo katika gesi ni upi?

Msimamo wa Profesa Muhongo mara baada ya kuteuliwa kuwa Waziri wa Nishati na Madini ulikuwa ni kutaka kupitishwa kwanza kwa sera ya gesi asilia kabla ya kuendelea na ugawaji wa vitalu vya gesi.
Septemba 2012, Profesa Muhongo alisema;

“Some of the agreements are really shoddy and they need to be revoked” and “I can’t tolerate agreements which are not in the country’s interests but they benefit a few individuals”.
Tafsiri yake ni:

“Baadhi ya mikataba ni ya ovyo, na inahitaji kuvunjwa” na “Sitovumilia mikataba ambayo haina maslahi kwa nchi na inawanufaisha wachache”.
Tanzania orders review of all oil and gas exploration contracts

Baada ya hapo, Profesa Muhongo aliamrisha Bodi mpya ya TPDC kusitisha ugawaji wa vitalu vya gesi ambao ulipangwa kufanyika mwezi Septemba 2012 na kupitia upya mikataba yote. Profesa Muhongo alinukuliwa akisema:

‘Earlier this month, the state-run Tanzania Petroleum Development Corporation (TPDC) delayed a licensing round for nine deep-sea oil and gas blocks previously set for this month until a parliamentary vote on a new gas policy in October. "Right now as a country, we are in the gas boom and we don't have gas policy in place.”

[…]

Recent gas strikes off east Africa's seaboard have led to predictions the region could become the third largest exporter of natural gas on the planet.

"Our country is reviewing its policy. Is that something new?" he said. "We want both the companies that are investing in the country and Tanzanians to benefit from the oil and gas projects."

[…]

"This is completely new business to us. We are learning," Muhongo said.’
Tafsiri yake ni:

‘Mwanzoni wa mwezi huu TPDC ilihairisha mchakato wa ugawaji wa vitalu tisa vya gesi asilia vilivyoko baharini hadi hapo Bunge litakapopitisha sera mpya ya gesi iliyowasilishwa bungeni mwezi Oktoba;
"Kwa sasa kama Taifa, tuko katika mazonge ya gesi na hatuna sera ya gesi. 
"Nchi yetu inaandaa sera (ya gesi). Hicho ni kitu kipya?..." 
"Tunataka kampuni zote, kampuni zinazowekeza nchini mwetu na Watanzania tunufaike na miradi ya gesi na mafuta."
"Hii ni biashara mpya kabisa kwetu. Tunajifunza."

UPDATE 2-Tanzania says will not revoke any oil and gas PSAs | Reuters
Zoezi wa la kugawa vitalu vya gesi asilia lilisitishwa lakini hadi sasa matokeo ya kupitia upya mikataba hayajatolewa hadharani.

Miezi michache baadaye, Februari 26, 2013, Profesa Muhongo alisisitiza msimamo wake wa kutaka Tanzania kuwa na sera ya gesi kabla ya kugawa vitalu zaidi. Aliyasema hayo alipokua akihutubia mkutano uliofanyika Chatham House, mjini London. Mkutano huo uliopewa jina “Tanzania: An Emerging Energy Producer”. Ulikuwa na madhumuni ya:


“Tanzania is drawing growing attention as a pivotal country in East Africa for oil and natural gas exploration, having led the region in terms of new discoveries of natural gas in 2012. With known gas reserves of approximately 7.5 billion cubic feet, the potential to transform Tanzania's international standing and domestic electricity production is considerable. However, recent protests against the construction of a pipeline to Dar es Salaam highlight the challenges that Tanzania faces in ensuring that the benefits of its natural resources are widely felt.

Tafsiri yake ni:

“Tanzania inaonyesha kuja juu katika Afrika Mashariki kwa uvumbuzi wa mafuta na gesi asilia baada ya kuongoza kwa uvumbuzi wa gesi asilia mwaka 2012. Ikiwa na wastani wa futi za ujazo bilioni 7.5, ni dhahiri itasaidia Tanzania kupaa katika anga za Kimataifa na kusaidia uzalishaji wa umeme kwa matumizi ya ndani. Hata hivyo, vurugu za hivi karibuni kupinga ujenzi wa bomba la gesi kwenda Dar es Salaam inaashiria changamoto mpya ambazo Tanzania sasa inakabiliana nazo kuhakikisha kwamba manufaa ya gesi asilia yanawafikia watu wengi zaidi wa chini.”

Alichowasilisha Profesa Muhongo katika mkutano huo kwa ufupi kinapatikana katika tovuti hii;

Tanzania as an Emerging Energy Producer | Chatham House: Independent thinking on international affairs
Kama inavyonekana kwenye kiambatanisho, moja ya nyaraka aliyowasilisha Profesa Muhongo inaonyesha kwamba mchakato wa kuanza ugawaji wa vitalu ungeanza baada ya kupitishwa kwa sera ya gesi.
Hadi sasa hatuna sera ya gesi asilia.
Lakini jambo la kushangaza, Profesa Muhongo amebadilika na anataka vitalu vigawiwe kabla ya kuwapo kwa sera gesi.


Sababu za kubadilika kwa Profesa Muhongo hazina mashiko


Profesa Muhongo amenukuliwa na gazeti la Daily News la Agosti 31, 2013 akieleza sababu zake za kutaka vitalu vigawanywe kabla ya kupitishwa kwa sera ya gesi. Sababu kuu alizozisema ni tatu; (1) Ushindani wa soko na majirani zetu akitolea mfano wa Msumbiji (2) Sheria ya mwaka 1960 iliyoanzisha TPDC na Sheria ya Petroli ya mwaka 1980 kwamba zinatosha kusimamia ugawaji wa vitalu akimaanisha sera na sheria mpya zitafuata baada ya ugawaji wa vitalu; na (3) Watanzania hawana uwezo wa kuwekeza katika sekta hii akimaanisha waachiwe wageni peke yao.

Maelezo kwamba tunashindana na Msumbiji haya halalishi ugawaji vitalu kabla ya sera. Utafiti wa gesi asilia ni jambo linachokua muda mrefu, ndio maana TPDC wanaingia kwenye mikataba ya muda mrefu (isiyozidi miaka 11 kwenye utafiti na miaka 25 kwenye uchimbaji). Kwa hiyo kusubiri miezi michache ili Bunge letu liidhinishe sera, haiwezi kuathiri ushindani wa kibiashara. Hata nchi Msumbiji anayoizungumzia hivi sasa inapitia upya mpango wake wa uwekezaji katika gesi asilia na kuingiza sera na sheria mpya zitakazo simamia rasilimali hiyo. Katika mahojiano yaliofanyika na jarida la Africa Report mwezi Julai mwaka huu, Naibu Waziri wa Nishati wa Msumbiji, Mh. Abdul Razak Noormahomed, alisema madhumuni ya mabadiliko hayo ni kuwapa kipaumbele wananchi wa Msumbiji.

Mohojiano haya yanapatikana katika anuani ifuatayo:

Extractive industry: The goal is to give an edge to Mozambicans - Noormahomed | Interview). 
Kama nilivyoeleza hapo juu, mara baada ya Profesa Muhongo kuingia wizarani alisema kinaga ubaga kwamba sheria iliyopo haikidhi mahitaji ya sekta ya gesi asilia ndiyo maana akasimamisha ugawaji wa vitalu vya gesi na kuamrisha mikataba ipitiwe upya na sera ipatikane. Leo tunashuhudia Profesa Muhongo akila matapishi yake na kusema kwamba sheria zile zile alizoziponda sasa zinafaa.

Kauli ya Profesa Muhongo kwamba wafanyabiashara wa Tanzania wanaweza tu kushiriki biashara ya juisi na soda na hawana uwezo wa kushiriki katika biashara ya gesi yao ni dharau. Kigezo gani Profesa Muhongo anatumia kutoa kauli ya jumla yenye kutawaliwa na hisia? Amefanya utafiti gani kupima uwezo wa kifedha wa wafanyabiashara wa kitanzania? Kwa taarifa yake, wapo wafanyabiashara wengi ambao wanaweza kupata fedha kwa ajili ya kuchimba visima vya gesi. 
Ni dhahiri kwamba Profesa Muhongo anathamini tu kampuni za kigeni, anasahau kwamba kuna mifano ya kuwapo kampuni za kigeni ambazo zimekua zikifanya udalali hapa nchini kwa miaka mingi kwenye rasilimali za nchi yetu ikiwa ni pamoja na madini na gesi.

Uzalendo wangu:

Ningependa kupuuza tuhuma kwamba mimi si mzalendo Wantanzania wanafahamu ukweli. Vile vile ningependa kupuuza tuhuma kwamba mimi ni mbinafsi na sipendi maendeleo ya Watanzania wenzangu kwa hili pia Watanzania wanafahamu ukweli.

Kuhusu Kilimanjaro Hoteli na mgogoro na Yussuf Manji n.k, mtizamo wako unategemea wewe upo katika kundi lipi kati ya kundi safi la waadilifu au kundi chafu la wala rushwa. Watanzania wanafahamu msimamo wangu kwenye hili.
Mimi sipingi kuwepo kwa wawekezaje wageni katika sekta ya gesi lakini kuna mambo mawili napigania. Kwanza Watanzania wanufaike na rasilimali yao ya gesi na pili iwepo sera ya gesi inayotoa kipaumbele kwa Watanzania
Mimi napenda maendeleo ya nchi yangu; kwa hiyo hata siku moja siwezi kupinga uwekezaji ama ubia na wawekezaji. Ninachosimamia ni manufaa kwa nchi yangu.

Tuhuma kwamba nafanya kampeni dhidi ya wizara

Tuhuma kwamba nimeandaa kongamano kwa ajili ya vijana wa Chadema si za kweli. Huu ni uzushi usio na kichwa wala miguu. Vile vile madai kwamba naitumia vibaya vyombo vya habari vya IPP Media si ya kweli hata kidogo ikizingatiwa kwamba hata mahojiano ya Profesa Muhongo kwa simu akiwa Austria, yalirushwa na kituo cha redio cha Radio Stereo kinachomilikiwa na kampuni yangu ya ITV-Independent Television Limited.

Hitimisho

Julai mwaka huu, Rais wa Marekani Barack Obama, alihitimisha ziara yake ya Kiserikali nchini Tanzania, kwa kusema;

“Ultimately the goal here is for Africa to build Africa for Africans.”


Akimaanisha kwamba, Hatimaye Lengo ni Africa kujenga Africa kwaajili ya Waafrica

Profesa Muhongo asipingane na ushauri huu mzuri.
Nimalizie kwa kuwahakikishia Watanzania kwamba mashambulizi binafsi dhidi yangu yenye nia mbaya ya kunishushia heshima hayatakaa yafanikiwe.
Wenu,

Dk. Reginald A. Mengi

KAULI YA ISMAIL JUSSA KUHUSU KUMWAGIWA TINDIKALI PADRI MWANG'AMBA

KAULI YA ISMAIL JUSSA


Kwa mara nyengine tena leo hii kumetangazwa kutokea tukio la kumwagiwa acid ambapo imeelezwa jioni hii Padri Joseph Magamba amemwagiwa acid maeneo ya Sunshine Internet Cafe hapo Mlandege, mjini Zanzibar. Binafsi nalaani vikali kitendo hicho cha kinyama na cha kishenzi kabisa.

Juzi tu Jumatano nilisoma katika gazeti la Mwananchi tukio la mfanyabiashara wa vifaa vya ujenzi Christian Msema wa Mburahati, Dar es Salaam kumwagiwa acid na watu wasiojulikana waliokuwamo kwenye bajaj.

Matukio haya ni ya kinyama na ya kutisha na yanaonekana kushika kasi kila uchao. Bahati mbaya licha ya
 Polisi kutangaza operesheni maalum ya kutafuta kile walichokiita mtandao wa acid hakuonekani mafanikio yoyote.

Hivi uwezo wa uchunguzi wa Jeshi la Polisi umeshuka kiasi hichi? Na kwa nini hadi leo Serikali haijapiga marufuku uuzaji au upatikanaji mwengine wa acid ambao unaonekana kufanyika kiholela kiasi cha kupatikana kirahisi na kutumika kufanyia uhalifu kiasi hichi?

Yeyote au kikundi chochote kilicho nyuma ya matukio haya kinapaswa kulaaniwa kwa nguvu zote na kusakwa ili kuchukuliwa hatua kali dhidi yao.

Ismail Jussa
Muwakilishi – Mji Mkongwe