Sunday, September 15, 2013

KAULI YA ISMAIL JUSSA KUHUSU KUMWAGIWA TINDIKALI PADRI MWANG'AMBA

KAULI YA ISMAIL JUSSA


Kwa mara nyengine tena leo hii kumetangazwa kutokea tukio la kumwagiwa acid ambapo imeelezwa jioni hii Padri Joseph Magamba amemwagiwa acid maeneo ya Sunshine Internet Cafe hapo Mlandege, mjini Zanzibar. Binafsi nalaani vikali kitendo hicho cha kinyama na cha kishenzi kabisa.

Juzi tu Jumatano nilisoma katika gazeti la Mwananchi tukio la mfanyabiashara wa vifaa vya ujenzi Christian Msema wa Mburahati, Dar es Salaam kumwagiwa acid na watu wasiojulikana waliokuwamo kwenye bajaj.

Matukio haya ni ya kinyama na ya kutisha na yanaonekana kushika kasi kila uchao. Bahati mbaya licha ya
 Polisi kutangaza operesheni maalum ya kutafuta kile walichokiita mtandao wa acid hakuonekani mafanikio yoyote.

Hivi uwezo wa uchunguzi wa Jeshi la Polisi umeshuka kiasi hichi? Na kwa nini hadi leo Serikali haijapiga marufuku uuzaji au upatikanaji mwengine wa acid ambao unaonekana kufanyika kiholela kiasi cha kupatikana kirahisi na kutumika kufanyia uhalifu kiasi hichi?

Yeyote au kikundi chochote kilicho nyuma ya matukio haya kinapaswa kulaaniwa kwa nguvu zote na kusakwa ili kuchukuliwa hatua kali dhidi yao.

Ismail Jussa
Muwakilishi – Mji Mkongwe

No comments:

Post a Comment