Friday, September 27, 2013

MPANGO WA USHAURI WA BIASHARA

CPM Business Consultants imeandaa mpango kabambe wa ushauri wa biashara (Mentorship) kwa wafanyabiashara wadogo wa kati na wakubwa na wale wanaotaka kuanzisha biashara ili kuwawezesha kuwa wafanyabiashara wakubwa na wenye mafanikio. Mtu atakakayejiunga na mpango huu atapewa mbinu za hali ya juu za biashara na uwekezaji ambazo zitamuwezesha kuinuka kiuchumi na kuwa mfanyabiashara mkubwa kwa haraka. Mtu yeyote anaweza kujiunga na mpango huu ambao mkataba wake utakuwa ni wa mwaka mmoja mmoja ambao unaweza kurudiwa tena.Kwa nini uchague CPM Business consultants? Tumeweza kuwainua wajasiriamali wengi kwa ushauri wetu. Kitabu chetu cha Mbinu za biashara na maarifa ya kupata pesa na utajiri, kimewainua wajasiriamali wengi wengine ndani ya muda wa miezi 6 hadi mwaka mmoja. Pia tumefanikiwa kuuza nakala 4,000 za kitabu hicho kwa kipindi kifupi kwa sababu kinapendwa sana. Tumeweza kuandaa mpango wa biashara/michanganuo kwa wale walioomba mikopo Benki. Katika kipindi cha miaka 3 iliyopita tumewawezesha wateja wetu kupata mikopo ya sh. milioni 400 toka benki.
Manufaa ya kujiunga na mpango huu;
Utapewa mbinu za hali ya juu za biashara na uwekezaji ambazo zitakuwezesha kuinuka kiuchumi na kuwa mfanyabiashara mkubwa kwa haraka.
Utapata kitabu cha ujasiriamali kilichotungwa na Mshauri wa biashara.
Utajiunga na mafunzo maalum ya ujasiriamali kwa email kipindi chote utakachokuwa umelipia michango.
Utapata ushauri kwa kipindi cha mwaka mmoja bila kulipia gharama yoyote na unaweza kumpigia simu mshauri wakati wowote na kupatiwa ushauri.
Utapewa huduma ya kutangaza biashara yako kwenye mtandao wa Internet wenye wateja 50,000 bila gharama ya ziada.
Utapata ushauri wa kisaikolojia na matatizo ya mahusiano na maisha yanayokukabili.
Gharama ya mpango huu ni Sh. 25,000.00 Elfu ishirini na tano kwa mwaka. Ili kuomba kujiunga na mpango huu tuma sh. 25,000 kwa M PESA kwenye simu namba 0755394701, Kwa maelezo zaidi unaweza kupiga simu au kutuma email kwa cnazi2002@yahoo.com
Tumeamua kutoa bei ndogo tofauti na tangazo letu la mwanzo kutokana na maombi ya wadau wengi kuutaka mpango huu kwa gharama ambazo wanaweza kuzimudu.
CHARLES NAZI
MSHAURI WA BIASHARA
CPM BUSINESS CONSULTANTS

1 comment: